Sunday, May 19, 2013

MARIKEBU


Marikebu iliotengenezwa kwa kutumia mbao

Marikebu ilio tengenezwa kwa kutumia vyuma

Tafauti ya vyombo hivi viwili vya baharini ni kwamba kimoja kimetengenezwa kwa mbao chengine kwa  chuma,lakini bila shaka kazi zake ni moja,vyombo vyote vya olea juu ya maji na vyote hutumika kwa usafiri na pia kwa kufanyia biashara mbalimabli katika dunia yetu hii ili kujikimu kimaisha.


Kilichonifanya nipitie hoja hii leo ni jambo ambalo huwa lanikera kila siku,si kwa ubaya lakini hunikera kimawazo ndiposa leo nikaonelea nilijadili na nyie wenzangu ili tuzidi kutafakari na kupeana nasaha.

kwa ufupi mimi naishi sehemu inayo itwa likoni,kuja kwangu kazini kila siku mimi na wengi wengineo tunaoishi sehemu hiyo ya mombasa kusini lazima tutumie kivuko kiitwacho likoni ferry.Katika kivuko hichi kuna marikebu zinazo itwa ferry ,kwa hio wakati tunapovuka huwa twapata fursa ya kuona marikebu nyengine(meli)zikiiingia au kutoka bandari ya mombasa kwa niaba ya kufanya biashara mbali mbali.

wakati mwingi meli inapo pitia karibu na ferry;nishasikia wengi wa abiria wakisema, "aah bwana usicheze na mtu mweupe ",yaani kitu kikubwa hivi na kimesheheni mizigo mingi bila kuzama ambapo ukitupa shillingi,au msumari baharini kinazama.

Hii ndio hoja ambayo huwakanganya watu wengi,si makosa kufikiria namna hiyo na wala mimi siwakosoi kwa hilo,bali najua kuwa wazimu wa mtu ndio akili yake.

Bila shaka katika sisi wanadamu wa dini zote tushasikia mtume wa Mwenyezi Mungu alokua akiitwa NUHU.twaelezewa kuwa mtume huyu aliishi miaka 950 akilingania watu wafuate  dini ya mwenyezi MUNGU moja lakini watu wake walikuwa wapinzani sana hivi kwamba walio sikiliza maneno yake hawakufika hata 200.

Baada ya kulingania watu kwa miaka yote hiyo,mwenyezi MUNGU alimuashiria mtume wake kuwa kuna mda fulani yeye ataleta gharka ili awaadhibu wale wabaya,hapo ndio mwenyezi MUNGU alimuamrisha NUHU  atengeneze marikebu kwa jina SAFINA(Noah's Ark) ili ifikapo wakati wa hiyo gharka wasalimike yeye na watu wake pamoja na wanyama.kwani gharka yenyewe ilikuwa mvua kubwa ambayo ilileta mafuriko makubwa na kuangamiza vitu na watu.

Baada ya kisa hicho cha mtume NUHU Mwenyezi MUNGU yuasema aliifanya hiyo safina ya NUHU mpaka leo ili iwe kumbukumbu kwa watu wenye kufikiri.Katika wazimu wangu au fikira zangu chache nami nionapo meli ikiolea hunijia wazo kuwa hii ndio kumbukumbu ya marikebu ya NUHU ambayo iliolea na watu pamoja na vitu vyengine.

Je wenzangu kama nilivyo tangulia kusema awali kwamba mimi si kosoi mtu,kwani wazimu wa mtu ndo akili yake ,je haya ya marikebu kuolea juu ya maji na kubeba shehena za mizigo mikubwa mikubwa ni ujuzi na akili ya mtu mweupe  au chanzo cha wazo hili la marikebu ni wapi ?.


Huu ni ulimwengu na malimwengu yake...............




Thursday, May 2, 2013

MIAKA MITANO IMEPITA


Mawio au kupambazuka kwa jua eneo la likoni shelly beach.je kupambazuka kwa jua kila siku kunakupa taswira gani kama kiumbe?

Ni miaka mitano imepita sasa tangu nianzishe blog hii, nashkuru mwenyezi mungu kwa kunipa nafasi ya kuwa na afya njema mda wote huo mpaka kufikia leo ninapoandika tena kwenye blogi hii.

Nimeweka picha hii ya mawio kama ishara ya mwamko mpya ,kuashiria kuwa licha ya kuwa kimya mda wote huo bado niko na nia ya kuendeleza malengo yango ya kusoma na kuelimishana na wengine kupitia mtandao.

Kama munavyojua kuna ulimwengu na malimwengu.Ulimwengu na hii sayari tunayoishi sisi sote kama viumbe,na malimwengu na vitendo au yale yote yanayotusibu sisi kama viumbe.

Hii blogi nimeiita malimwengu kwa lengo la kujuzana mengi yanayo tuhusu au kutusibu kama waja wa mwenyezi mungu.Katika malimwengu kuna furaha,majonzi,njaa,shibe,uzima,ugonjwa na mengi mengineo  ambayo twaweza kuyajadili.

Ni furaha yangu kuwaalika wasomaji wangu katika mjadala wazi kuhusu malimwengu na ulimwengu wote.

Monday, May 25, 2009

karibuni

welcome once again to my blog,on this blog i would like a many comments as possible on how to improve the swahili part of my website www.swabak.com/malimwengu any idea on how to improve it and muchmuch more.

karibuni kwenye hii blogi ya malimwengu kwenye blogi hii ningependa kubadilishana mawazo tofauti jinsi nitakavyo fanya mtandao huu uwe wa kuvutia na pia uwe wa kuelimishana na mengi mengineo.
asanteni na karibuni

Saturday, March 21, 2009

karibuni

welcome to swalehes blog..........feel free to share in this blog...


welcome to my blog hope to share with as many people as possible in this blog ,mine is to say welcome and have a nice time