Marikebu iliotengenezwa kwa kutumia mbao
Marikebu ilio tengenezwa kwa kutumia vyuma
Tafauti ya vyombo hivi viwili vya baharini ni kwamba kimoja kimetengenezwa kwa mbao chengine kwa chuma,lakini bila shaka kazi zake ni moja,vyombo vyote vya olea juu ya maji na vyote hutumika kwa usafiri na pia kwa kufanyia biashara mbalimabli katika dunia yetu hii ili kujikimu kimaisha.
Kilichonifanya nipitie hoja hii leo ni jambo ambalo huwa lanikera kila siku,si kwa ubaya lakini hunikera kimawazo ndiposa leo nikaonelea nilijadili na nyie wenzangu ili tuzidi kutafakari na kupeana nasaha.
kwa ufupi mimi naishi sehemu inayo itwa likoni,kuja kwangu kazini kila siku mimi na wengi wengineo tunaoishi sehemu hiyo ya mombasa kusini lazima tutumie kivuko kiitwacho likoni ferry.Katika kivuko hichi kuna marikebu zinazo itwa ferry ,kwa hio wakati tunapovuka huwa twapata fursa ya kuona marikebu nyengine(meli)zikiiingia au kutoka bandari ya mombasa kwa niaba ya kufanya biashara mbali mbali.
wakati mwingi meli inapo pitia karibu na ferry;nishasikia wengi wa abiria wakisema, "aah bwana usicheze na mtu mweupe ",yaani kitu kikubwa hivi na kimesheheni mizigo mingi bila kuzama ambapo ukitupa shillingi,au msumari baharini kinazama.
Hii ndio hoja ambayo huwakanganya watu wengi,si makosa kufikiria namna hiyo na wala mimi siwakosoi kwa hilo,bali najua kuwa wazimu wa mtu ndio akili yake.
Bila shaka katika sisi wanadamu wa dini zote tushasikia mtume wa Mwenyezi Mungu alokua akiitwa NUHU.twaelezewa kuwa mtume huyu aliishi miaka 950 akilingania watu wafuate dini ya mwenyezi MUNGU moja lakini watu wake walikuwa wapinzani sana hivi kwamba walio sikiliza maneno yake hawakufika hata 200.
Baada ya kulingania watu kwa miaka yote hiyo,mwenyezi MUNGU alimuashiria mtume wake kuwa kuna mda fulani yeye ataleta gharka ili awaadhibu wale wabaya,hapo ndio mwenyezi MUNGU alimuamrisha NUHU atengeneze marikebu kwa jina SAFINA(Noah's Ark) ili ifikapo wakati wa hiyo gharka wasalimike yeye na watu wake pamoja na wanyama.kwani gharka yenyewe ilikuwa mvua kubwa ambayo ilileta mafuriko makubwa na kuangamiza vitu na watu.
Baada ya kisa hicho cha mtume NUHU Mwenyezi MUNGU yuasema aliifanya hiyo safina ya NUHU mpaka leo ili iwe kumbukumbu kwa watu wenye kufikiri.Katika wazimu wangu au fikira zangu chache nami nionapo meli ikiolea hunijia wazo kuwa hii ndio kumbukumbu ya marikebu ya NUHU ambayo iliolea na watu pamoja na vitu vyengine.
Je wenzangu kama nilivyo tangulia kusema awali kwamba mimi si kosoi mtu,kwani wazimu wa mtu ndo akili yake ,je haya ya marikebu kuolea juu ya maji na kubeba shehena za mizigo mikubwa mikubwa ni ujuzi na akili ya mtu mweupe au chanzo cha wazo hili la marikebu ni wapi ?.

